Kwa
muda mrefu kikundi cha wahuni kilijaribu na kufanikiwa kupoka madaraka ndani ya
Chama cha Mapinduzi. Watu hawa walitaka kujijengea "cartel" ya
kuongoza nchi, humo walikuwemo watu kadhaa na hasa wafanyabiashara akiwemo
Lowassa na yeye ndiye alikuwa Msanifu wa genge hilo na hasa ili kutimiza ndoto
yake ya kuwa Rais hata kwa kuununua Urais wa nchi yetu, alifanya hivyo mwaka
1995 akashindwa maana Mwalimu alikuwepo. Baada ya hapo genge hili
lilijiposition kwenye maeneo yote nyeti ya nchi yetu.
Mwaka
huu wana CCM tumekataa upumbavu huu wa kudhani Urais na Uongozi unaweza
kununuliwa kama nyanya. Tumekataa na tumehakikisha katika ile
"CARTEL" au GENGE la WAHUNI hakuna kati yao ambaye anaiona IKULU kwa
tiketi ya CCM. Imewauma sana, Huyu bosi ndio kaenda UKAWA na wako waliobaki
CCM, tutashughulika nao strategically, lakini kwanza ni lazima tupate Rais
Mwadilifu KWANZA ambaye atatusaidia kazi ya Pili ya Kusafisha UFISADI. kazi ya
Kwanza imekuwa kuwanyima Dhamana ya Urais kupitia CCM.
Hapa
CCM wanapaswa kwakweli kujitoa kimasomaso. GENGE sasa limehamishia mapambano
kutoka Kambi ya Upinzani. Utagundua hoja ya UFISADI ilishamiri sana na ndio
maana kipindi fulani UKAWA waliunga Mkono kazi yetu ya Katiba ambayo lengo lake
lilikuwa kuja kuua CARTEL au GENGE la WAHUNI, leo UKAWA hawana tena uhalali
(legitimacy) ya kukemea UFISADI maana UFISADI umetamalaki kati na juu yao.
Hebu
tafakari mtu kama ndugu yangu na kaka yangu Saeed Kubenea kwa kazi yooote
aliyofanya miaka nenda rudi mpaka akashambuliwa, juzi alijisikiaje pale kawe
aliponyooshwa mkono juu na Edward Lowassa? Dhamira yake ilimweleza nini? Na
Lowassa hakusita kumpiga kijembe kwamba huyu alikuwa machachari sana kwenye
Media sasa apunguze, hivi Kubenea amejiuliza Lowassa alimaanisha apunguze nini
na kwa faida ya nani.?
Mimi
mpaka TV mbili kubwa zimekataa nisikaribishwe kwenda kwenye vipindi kwa
maelekezo ya wamiliki. Je kukataliwa kwangu ni kwa faida ya nani? Mbona kama ni
siasa kila siku kwenye TV hizo wadau wa UKAWA wanajimwaga vilivyo, je mimi
tatizo langu ni nini? Wengine walifurahia TCRA kutoa tamko la kukataza watu
kwenda kwenye vipindi vya moja kwa moja, na wengi walisema mitandaoni
wamenikomesha mimi, hivi mimi nikikomeshwa ni kwa faida ya nani?
TCRA
walilazimisha kwamba ili uruhusiwe kushiriki kwenye vipindi vya moja kwa moja
ni lazima uwe mwakilishi wa vyama vya siasa. Mimi nikasema kwa hakika
ningemwambia ndugu Kinana Katibu Mkuu wa CCM angenipa barua ili niendelee
kushiriki. Lakini nikasema hivi wanaoruhusiwa kushiriki ni wanasiasa peke yake?
Je uchaguzi ni haki uhodhiwe na wanasiasa pekee? Nikaendelea kujiuliza hivi
uchaguzi mkuu wanaotakiwa kujadiliana zaidi ni Wananchi wanaochagua ili kutoa
dhamana au wale wanaoomba kuchaguliwa ili kupewa dhamana? Nikasema mbona Katiba
inasema kuna Uhuru wa kuweka mawazo hadharani je mawazo hayo yako limited
wamakati wa uchaguzi?
Nikafunga
safari kwenda TCRA nikawauliza maswali hayo na namshukuru Mungu aliwapa busara
kubwa na baadaye walitoa tamko kubatilisha katazo lao la awali. Lakini
nikajiuliza zaidi kwanini hata wale wadau wa asasi za kiraia hawakuoneshwa
kukasirishwa na kitendo kile cha TCRA? Nikasema hata watu wote wakisimama mimi
nitaendelea kudai haki na kweli katika nchi yangu.
Leo
siwezi kwenda kwenye TV mbili kubwa na wamiliki wameweka msimamo, kwanini? Wale
wanaofurahia mimi kukataliwa je wanapata faida gani.? Mbona mimi nikionana na
vijana na wadogo zangu ambao wako katika vyama vya upinzani nawapa moyo na
kuwaambia watende sawasawa na dhamira zao njema na kwamba walitizame Taifa
kwanza? Najiuliza je Tatizo langu ni nini? Au sijitambui? Au niko naïve?
Nitasema
kweli Daima na fitina kwangu mwiko na nitatumia elimu yangu kwa manufaa ya Wananchi
wa Taifa langu. Kwanini leo baadhi ya watu wamenigeuka, watu ambao walifurahia
nilipowaambia pale Ubungo plaza na pale Mlimani city kwamba maslahi binafsi
yanahatarisha mustakabali wa Taifa letu. Nilikwenda mbali na kuwataja watu hao
na watanzania baadhi na wengi wakanifurahi sana. Mbona leo naendelea kuwasema
watu wale wale na baadhi ya watanzania wananiona nimegeuka? Kwanini waliniamini
kipindi kile na wakijua mimi ni CCM na nilikuwa nawasema CCM na leo Mimi nikiwa
bado CCM nawasema watu ambao wanataka kutununua ili waendeleze GENGE la KIHUNI
mbona watu wanaema mimi ni kigeugeu? Naendelea kutafakari.
Siku
moja nilikaa na viongozi wawili wa CCM, mmoja akasema nadhani mchakato wa
Katiba ni lazima kabla ya kura ya maoni tujenge muafaka na kufanya maridhiano
ili kila sauti ya Mtanzania isikilizwe. Kiongozi mwenzake mdogo kidogo kwa cheo
akabisha sana na akasema ni lazima twende kwenye kura ya maoni kwasababu tendo
la Katiba kwa lilipofika ni kama maji yanayomwaga kutoka katika bilauli kwamba
ni lazima yafike chini.
Nikamtazama
na kumkazia macho na nikamweleza wacha na mimi nizungumze kama mwana CCM.
Nikawaomba niwaeleze historia ndogo ya namna nipo nilipo. Nikasema nianzie
kwenye Katiba, nikawaambia unajua mimi nilikuja Tume ya Katiba nikiwa simfahamu
mtu yeyote isipokuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano? Nikawaeleza mimi sikumfahamu
Mzee Warioba, Jaji Ramadhani, Mzee Butiku, Dkt. Salimu wala Profesa Kabudi na
wengineo, sikumfahamu hata mmoja. Nilikuwa namfahamu Rais Kikwete tu. Alipotupa
kazi na akatuagiza tuwasikilize watanzania na watakachosema ndicho ambacho
tukiandike, tulifanya hivyo kwa unyenyekevu mkubwa kwa watanzania.
Hata
pale ambapo Rais alionekana kutoka na msimamo tofauti na wetu nilibaki
kuwaambia watanzania kwamba Tanzania njema itajengwa na watanzania wenyewe.
Hatukuishia pale tuliokuwa wajumbe wa Tume ya Katiba tulifanya utafiti kwa
kuzungumza na wadau mbalimbali, wabunge, viongozi wastaafu, watu mashuhuri ili
kuelewa tatizo lilikuwa wapi.
Utafiti
huu wa chini chini ulinipa fursa ya kuonana na wabunge wengi wa CCM na wa
upinzani na wote walikiri kwamba “Bwana Mkubwa amekataa” na tulipozidi kuhoji
hoji tulikuja kukutana na wapambe wake kwanza ambao walisema “tatizo lenu
mmedhoofisha Urais na kwamba Kikwete anataka kuondoka ameweka masharti na
kanuni ngumu za uongozi hilo haliwezekani” wakaendelea kusema “yeye (Kikwete)
aende na sisi tubaki na madaraka yale yale au zaidi na tuwe na mamlaka kama
aliyonayo sasa katika nchi”.
Wapambe
hawa tulizungumza nao kwa maana ya kuwapa elimu ya Rasimu ya Katiba na wakawa
wanatuuliza “kwahiyo ninyi (Tume ya Katiba) mnashauri ‘Mkubwa’ achukue Urais wa
Tanzania au Urais wa Tanganyika?” Tukasema achukue ya Muungano, wakasema “je
itahusisha madini, gesi na ardhi”? Tukasema hapana, wakaendelea kuuliza “je
akichukua ya Tanganyika atakuwa na uwezo wa kusafiri nje ya nchi kama Rais
Kikwete na kupigiwa mizinga 21”? Tukasema hapana, mmoja wao akasema “anhaaa
hapo ndio mnapokosea, sisi tunataka zote za Tanganyika na Muungano ziwe pamoja”,
kwa kusema hivyo walikuwa wanamaanisha serikali mbili.
Hatukuchoka
tukafanya utaratibu na tukaenda kumuona “Bwana Mkubwa” yaani Edward Lowassa, tulikutania
ofisini kwake mikocheni. Ili kuweka uwazi katika mkutano ule tulijumuisha pia
wawakilishi watatu wa Asasi za Kiraia na Makamishna Wawili, mimi nikiwa
mmojawapo, tulikuwa na kikao ambacho hakikupungua saa mbili.
Ni
katika kikao kile nilithibitisha kwamba aliyebuni mkakati wa kuikataa Rasimu ya
Warioba kwa CCM alikuwa Edward Lowassa tena akaonesha kufurahishwa na Rais
Kikwete kama Mwenyekiti wa Chama kuzomewa na hatimaye Rasimu aliyoipeleka
katika Chama kukataliwa. Nilijuliza sana mimi kama Kiongozi kijana, tafsiri
yake ni nini? Huyu ni mwana CCM na anafurahia Mwenyekiti wake kudhihakiwa na
kutupiwa Rasimu yake katika kikao. Leo najiuliza kama alikuwa na dhamira ya
kuikubali rasimu ya Warioba kwanini alikaa kimya wakati Mwenyekiti wake
akidhihakiwa?
Nikawaeleza
iliyokuwa Tume ya Katiba iliwahi kumwita hata mzee Kingunge aje tujadiliane
kuhusu Rasimu ya Warioba na alipokuja aliwatukana wajumbe wa Tume pamoja wageni
wengine waalikwa akiwemo Profesa Sherrif kutoka Zanzibar, nilipoona anamwunga
mkono Lowassa sasa namwelewa na ndio maana katika mkutano wa Taasisi ya Mwalimu
Nyerere nilidiriki kusema Mungu akinipa umri mrefu na kufikia uzee namwomba
Mungu nisiwe kama wao.
Nikamwambia
yule Kiongozi mdogo, unadhani ni kazi rahisi mimi kama kijana mdogo kusimama
kidete kutetea maoni ya Wananchi? Nilijua aliyekuwa na maslahi katika kutupilia
maoni ya Wananchi hakuwa Kikwete bali Edward Lowassa ambaye amekuwa akiutafuta
Urais wa kifalme. Kuthibitisha hilo nilimtamka kwa jina mara kadhaa Ndugu
Edward Lowassa kwamba hafai kuwa Rais wa Tanzania.
Na
kwangu mimi nilikuwa najiuliza hata kupitia CCM ambako mimi ni mwanachama,
iweje mtu ambaye anakosa kuheshimu watanzania wanapotoa maoni yao ya Katiba akawa
ni mtu ambaye atasimama ili wampe dhamana ya kuwa Rais wao. Mimi nilimkataa tangu
CCM na nilipoona CCM kama vile wanachelewa, mimi (Polepole), Mzee Butiku na
Mzee Warioba tulifanya mdahalo na tukaweka msimamo kama Lowassa atapewa tiketi
ya kugombea Urais kupitia CCM basi sisi watatu tusingejitoa bali tungepiga
kampeni ya kusema CCM isichaguliwe.
Nikaendelea
kumwambia hili la Katiba Mbaya wake namjua na alijaribu kuhonga watu, ni lazima
tujenge muafaka wa kitaifa kwanza. Namshukuru Mungu Kiongozi Yule ni muelewa
akasema muafaka ni kitu muhimu, hilo linawezekana na ni kwa maslahi ya
watanzania wote sema tu kipindi kile kiligubikwa na ushindani wa kisiasa, ila
sasa ni muhimu tukaja pamoja kama Taifa. (Mwisho wa kunukuu kikao change na
viongozi wa CCM)
Uhalisia
huu ndio umefanya Mzee Joseph Sinde Warioba kupiga kampeni ya Chama cha
Mapinduzi. Ila kitu kimoja napenda kuwaeleza kuna maadui ndani ya CCM na nje ya
CCM na hasa hasa wale ambao wako chini ya “cartel” au lile GENGE la WAHUNI
ambalo linafanya kila jitihada ili Mgombea wa CCM asiye na makundi na asiye na
msalie mtume na wezi, wabadhirifu na mafisadi. Maadui hawa wako radhi Mwana
Mtandao mwenzao (aliyeondoka CCM na kwenda UKAWA) apewe dhamana ya Urais wa
nchi yetu ili waendelee kutunyonya kwa maslahi yao.
Ikumbukwe
UKAWA huu sio UKAWA ule ambao mimi na Mzee Butiku na Mzee Warioba tulifanya nao
kazi pamoja, si hawa. Hawa UKAWA wa sasa ni watu wenye uchu wa ajabu wa
madaraka na kwamba wako tayari kumtumia mtu mwenye nasaba zote na ufisadi ili
awafikishe ikulu.
Kama
ni masikini na nikaambiwa mwabudu shetani ili niwe tajiri, nitakataa na kutunza
utu wangu kama ambavyo Bwana Yesu alikataa kumwabudia shetani kwa sababu
hizohizo.
Hivi
sielewi hawa wanachama wa Chadema ambao wamekubali kumeza matapishi yao wenyewe,
wanapataje amani mioyoni mwao wanapojua mgombea Urais wao ndio Yule mtu
waliyesema ni fisadi kwa zaidi ya miaka 8. John Mnyika alisema anao ushahidi wa
UFISADI wa Lowassa, Mbowe alisema anashangaa vibaka wanachomwa moto na Lowassa
ameachwa anadunda mtaani, Mchungaji Msingwa aliyesema anayemkubali Lowassa
akapimwe akili na Godbless Lemay eye amekuwa kimya kidogo ila naye amesema ni
halali kumtupia jiwe fisadi lowassa. Hawa leo wanapataje uthubutu wa kusimama
katika jukwaa moja na Lowassa na tena wakainuliwa mikono akiwanadi.
Mimi
nilijiapiza wale waliokataa maoni ya Wananchi sitaki urafiki nao hata leo, na
Lowassa ni mfano mmoja. Na niko tayari kuendelea kuunga mkono mabadiliko chanya
yaliyofanywa na Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa kuuvunja na kuwanyima Urais
kupitia CCM. Hii ndio CCM ya kweli, CCM ya wakulima na wafanyakazi, CCM
inayochukia rushwa katika uongozi na sasa tumeanza na Urais na baada ya Urais
tutawashukuia wabaya wote waliosalia. CCM ambayo haishurutishwi na matajiri
wanaotaka kututengenezea viongozi ikiwemo nafasi ya Urais.
ITAENDELEA
ovyoooooo
ReplyDeleteEndelea tu kuongea kadri utakavyo lakini baada ya Octoba 25 tutataka uendelee kuongea kama hivi hivi.
ReplyDeleteThanks polepole, ni kero sana kushabikia uraghai, cdm niwaraghai
ReplyDelete